PUNGUZA MANYAMA UZEMBE....

NO MORE MANYAMA UZEMBE!!!!!!!!
*****KWA DAWA ZA KUPUNGUZA TUMBO NA MANYAMA UZEMBE WASILIANA NA FETTY KWA SIMU NAMBA +255 767 728 764*****
Utatumiwa Popote Ulipo, Just call/ WhatsApp Or Sms +255 767 728 764

Matangazo

Kwa Matangazo Wasiliana Nasi Kwa 0753 891 997

Monday, November 10, 2014

TEAM WEMA WAKINUKISHA IG...NI MAMBO ZA MA'PROJECT TUU SASA!!!

Habari zenu wapenzi wa mie!!!
Duh, nimeona nisimalize siku kabla sijawapa huu ubuyu(hot news) zilizojiri na zinazoendelea kutikisa huko Instagram....

Baada ya uvumi wa muda kuwa Wema Sepetu kampiga chini our shem darling ''Diamond Platnumz'' sasa naona si uvumi tena ila ni mambo hadharaniiiii...
Maana ukishaona mtu amepatana na X wa mtu wake ujue na yeye ameshakuwa X... So hapo No bifu.. Hahahaaaa!!!!

Penny & Wema In Birthday party ya shostito wao!!!

(Which kwa mie naona it's very nice, hongereni wadada kwa kuamua kuweka tofauti zenu pembeniiii)

Team Wema pia wameonekana kufurahishwa sana na kitendo cha Wema na Penny kuwa marafiki kama zamani, ila sasaaaa sakata liliibuka baada ya Mwanadada wa ki'ganda  maarufu kama Boss lady (Zari) ambaye inasemekana ni mwanamke tajiri kuliko wote East Africa alipo'post picha kuwa amekutana na shem darling kwenye ndege from S.Afica to Tz....
 
Hapa kila mtu alichukulia kawaida tuu!!!

Haikuwa noma saaaaana kwa siku hiyo maana at the end of safari Zari alijishaua kwa maneno hayo...

Na hamna aliye'spread umbea wowote hadi hapo...
Kesho yake sasa ndio mambo za ma'project zilipoanza na Zari ali'post tena picha nyingine kumshukuru shem darling for a new project.....
 
 Project ilikuwa na picha tata kidogo... Hapa nyingine sijazipata ila shem darling alikuwa katika ma'pose tata na Boss Lady Zari.. Mmmmh!!!

 Hapo sasa wa'bongo wakawaza... Diamond anatuchezea akili.. Alivyommwaga Penny kimya kimya na kurudisha majeshi kwa Wema wali'post picha tata na kusema wana'act movie China... Hahahahaaa!!!
So wakaona huyu ni tabia yake, wamemwagana na Wema kimya kimya sasa wana'post picha tata wanadai ni project!!!

Je ni kukutana tuu kwenye ndege by coincidence na kupiga ma'selfie ya hatari ndio kumezua ''project'' ya faster namna hii?????

Baada ya team Wema kujipa majibu yao wenyewe sasa wakacharukaaaaaaaaa.....

Hahahahaaaaa....bila shaka hapo Zari alijutaaaaa kuwafahamu wabongo, maana walimzodoa hadi mie nikamuonea huruma
 Yaani walimchamba na matusi makubwa makubwaaa... nimeona hadi aibu kuyaweka huku... Wamemtukanaaaaa hadi akatukanika maskini....

Baadhi walimuonea huruma na wengi waliitana kushuhudia ubuyuuuu!!!!

 Sasa kila mtu ndio akawa kalishikia bango swala zima la ''project'' Hahahahaaaa!!!

Utashangaa kama wewe bado hauna ''project'' mwaka huu!!!

Wema nae huyu apa ame'chill na Penny and their friend...
 
 

Tisa kumiiiii, Wema na Penny nao wakaungana na kuendeleza issue ya the project...hahahahaaaa!!!
Shem darling umekomeshwaaaajeeeee!!! Ila umetia hurumaaa, kama nakuona roho inavyokudunda...lol!!!
Chezea wanawake uwazunguke then wakushtukie alafu sasa wamekuona wewe ni gaddem mbululaaaa... Kwa raha zao wamepatanaaa na kinachofuataaaa ni .....................!!!!!
Utasemwa mwanzo mwishoooo.... Pole na koma kwa tabia yako mbaya shem darling wa zamani!!!

 
 Penny nae alimuunga Wema mkono kwa ku'repost hiyo post... Hahahahahaaaa.... 

Jamani ni full rahaaa... Ila sasa team Wema mmenishangaza kitu kimojaaaaa tuuuu... Kama Wema ndie alimtema shem darling, na yeye mwenyewe kajisemea yupo at peace... Iweje mumtukane ivo mdada wa watu??? Eeeeh, au hamtaki shem darling ajipatie ''project'' nyingine???? Na ni kwa Zari tuu au kwa yeyote atakayekuwa nae mtakuwa mnamponda ivooo??? 
Msije fanya wadada wakaogopa kum'date tena shem darling jamaniiiii.... Hahahahahaaaa!!!

Mwisho niseme ukweli, Wema nakutamani aiseee, yaani una Team kabambeeee, inakupenda upendo wa kiukweliiii... Maana mtu tuu akigombana na wewe wanamkomeshaaa, and cha kushangaza wale wale wanaomkomesha mliyegombana nae, siku ukipatana nae nao haoooo wanahama na wewe na wanaanzaje kumpenda, kumsifu na kumpa full support na kusahau kabisaaaaa kama wao wao ndio waliokuwa wanamtukana mlivyokuwa hampatani.. Shikamooni Team Wema popote mlipo!!!! Nawakubali kinouma sana.....


Nawapenda mnooooooooooo!!!!!
XOXO.....

No comments:

Post a Comment

NGUVU DRINK

NGUVU = Nguvu Zaidi Ni Spirit Drink INGREDIENTS: Fine spirit, Gin flavour & Ionised water "Not For Sale To Person Under The Age Of 18" P.o.Box 54280, Dar es salaam,Tanzania

NGUVU SPIRIT AVAILABLE AT GF MIN-DEPOT