PUNGUZA MANYAMA UZEMBE....

NO MORE MANYAMA UZEMBE!!!!!!!!
*****KWA DAWA ZA KUPUNGUZA TUMBO NA MANYAMA UZEMBE WASILIANA NA FETTY KWA SIMU NAMBA +255 767 728 764*****
Utatumiwa Popote Ulipo, Just call/ WhatsApp Or Sms +255 767 728 764

Matangazo

Kwa Matangazo Wasiliana Nasi Kwa 0753 891 997

Saturday, August 16, 2014

UKWELI KUHUSU NDOA YA GARDNER NA JIDE

Dears,
Mimi kwa upande wangu namkubali sana Lady Jay Dee (Jide), i love her sense of fashions... Utakubaliana na mimi aisee Jide ni sooo in fashions....she got all the confidence na jinsi anavyovaa, she got no Rules at all...what matters ni kutoka bombaaa...  
It takes a couragous fashionista to put on Full Yellow...
Napenda jinsi anavyo'choose her hair styles. Yaani she is just ''herself'' na huwa hapendi awe kama wale wale mliowazoea..Yupo ki'Jide-Jide all the time and she is always doing better than before....
              

          
Shikamoo Jide, hata Rihana hakufikii kwa hair styles aiseee...

Napenda anavyo'maintain mwili wake... One of ''diet'' ninayotumia now kujipunguza uzito it's from her blog www.jidejaydee.com (mnaotaka kupungua pia muingie hapo mjifunze mbinu za kupungua)
Lady Jay dee akifanya mazoezi ya mwili

 
Ingieni kwenye blog yake mjue How to use this for weight loss...

Napenda nyimbo zake ever since nikiwa form two till now... Napenda anavyojishughulisha pia... In short, Jide ni mwanamke wa kuigwa for sure...

Gardner na Jide siku ya ndoa yao...
 Sasa kuna uvumi wa hizi siku mbili tatu, eti ndoa ya Jide na Gardner imevunjika.... Jamani jamani,mimi mwenyewe niliamini eti nikaanza na kuhuzunika kabisaaa. Lakini leo ndio nimeupata ukweliii..  Thanx wewe uliyenitumia huu ukweli wa mambo... umenitoa simanzi!!!
Ebu na wewe uliyekua na huzuni kama mimi jisomee apa....
 nimenukuhu...
''Ilisemekana kuwa taarifa za kuachana huko zinachochewa pia na baadhi ya maandiko ambayo Jide amekuwa akiyaweka katika akaunti zake za mitandao katika siku za hivi karibuni.
Ilielezwa kwamba katika akaunti yake ya Mtandao wa Istagram, Jide aliweka picha yake akiwa amesimama nje ya gari lake kisha akasindikiza kwa kuandika hivi: “Walking away from troubles”, maneno ambayo kwa tafsiri isiyo rasmi yanamaanisha kujiondoa kwenye matatizo.
Ilidaiwa kuwa kabla ya hapo, katika mitandao inaandikwa kuwa Jide pia aliweka picha yake akionekana kuwa na huzuni huku Binti Machozi akilengwalengwa na machozi na kusindikizia na maneno akiuliza: “Sijui nisemaje?”
Kufuatia tetesi hizo, gazeti la Ijumaa liliamua kuzifanyia kazi ili kupata ukweli.
Mtu wa kwanza kupigiwa simu alikuwa ni Gardner ambaye aliipokea na kabla hajaelezwa chochote, alisema alikuwa katika sehemu ambayo asingeweza kuzungumza, hivyo angempigia mwandishi wetu baada ya robo saa.
Baada ya kukata simu, mwandishi wetu alimwendea hewani Jide na baada ya kuita kwa muda, simu yake ilipokelewa na Gardner akasema: “Mpigie baada ya robo saa.”
Dakika ishirini baadaye, Gardner alimtumia ujumbe mfupi wa simu mwandishi wetu na kumweleza kuwa alikuwa Kituo cha Polisi Oysterbay, Kinondoni jijini Dar ambako aliitwa kwa ajili ya soo lao la kuwakimbia trafiki.
Baada ya kubadilishana maneno kadhaa, baadaye aliamua kupiga na mazungumzo kati yake na Ijumaa yalikuwa kama ifuatavyo;
Ijumaa: Ebwana hivi hizi habari kwenye mitandao juu ya kuvunjika kwa ndoa yako na Jide zimekaaje?
Gardner: Hamna kitu bwana, watu wanaunganisha tu vitu sijui kwa sababu gani.
Ijumaa: Sasa kama ni hivyo kwa nini Jide hakuja kukuona siku ile ulipolala polisi?
Gadner: Unaona sasa, wao wanajua hivyo, lakini siyo kweli, Jide alikuja usiku sana kwa sababu alikuwa anawaogopa mapaparazi.
Unajua Jide yeye huwa hapendi hayo mambo. Alikuja usiku sana, lakini hata hivyo polisi nao walimgombea sana kumpiga picha.
Ijumaa: Wanasema Jide kuna maneno amepost kwenye akaunti zake mitandaoni zinazoonyesha kuchoshwa na wewe, unasemaje?
Gardner: Si ndiyo kama hivyo nimekuambia, watu wanaungaunga tu vitu ambavyo hawavijui na sisi hata hatujui malengo yao.
Wakati ule uliponipigia simu mara ya kwanza nilikuwa naye kwenye gari ananipeleka pale polisi, lakini akapaki mbali kwa sababu hiyohiyo niliyokuambia kuogopa mapaparazi na si unakumbuka hata ulipompigia kwenye namba yake nilipokea mimi?
Ijumaa: Kwani upo naye hapo sasa hivi nimsalimie?
Gardner: Hapana tumeachana mimi niko kwenye usafiri mwingine naelekea kazini na yeye yupo kwenye misele mingine.
Ijumaa: Haya kaka basi poa.
Gardner: Poa kaka, mchana mwema.

 Mwisho wa kunikuhuu....
Jamani, unajua unaweza ukawa unasubiria mwenzio aachwe, matokeo yake ukaachwa wewe??? Hahahaaha... Sasa nyie mnaosubiria Jide na Gardner waachane basi mtasubiri sana, maana Gardner mwenyewe kashatuambia "mnaunga unga tuu vitu"
Wengine kuachana wanasemaga ni mpaka D-Day na wengine wanaiita Forever!

Mie apa nawa'love love woteee....
XOXO!!!

1 comment:

  1. Kama unansema vile hehehee team kujishuku

    ReplyDelete

NGUVU DRINK

NGUVU = Nguvu Zaidi Ni Spirit Drink INGREDIENTS: Fine spirit, Gin flavour & Ionised water "Not For Sale To Person Under The Age Of 18" P.o.Box 54280, Dar es salaam,Tanzania

NGUVU SPIRIT AVAILABLE AT GF MIN-DEPOT